Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, August 30, 2012

CRA yahitaji 6bn/ kuweka anuani Dar es Salaam



Na Kunze Mswanyama,DAR ES SALAAM
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inahitaji zaidi ya shilingi bilioni 6 ili kuweka anuwani za makazi kwa mkoa wa Dar es salaam pekee ikiwa ni gharama za ununuzi wa vitendea kazi, usafiri na mahitaji mengine ya lazima.

Hata hivyo,TCRA imeomba wananchi kuchangia zoezi hilo kwani kutokana na kupanda kwa gharama za bidhaa, mahitaji yanazidi kuongezeka na kwamba imepangwa kufanyika harambee maalum.

Katibu Mkuu wa wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Dk.Florens Turuka alipokuwa akitoa taarifa ya mradi huo mbele ya wandishi wa habari waliojumuika kwa pamoja na wabunge wote wa Dar es salaam.

Alisema, kwa kutambua umuhimu wa mradi huo viongozi wa jiji walikubaliana kwa pamoja kuandaa chakula cha hisani cha kuweza kuchangisha na kupata fedha za kuchangia utekelezaji kwa ufanisi na kwa muda uliopangwa.

“Serikali kwa kupitia TCRA imefungua akaunti maalumu kwa ajili ya uchangiaji mradi huo ili kutekeleza mfumo wa anwani za makazi katika mkoa wa Dar es salaam. Akaunti hiyo inaitwa TCRA-Postcode Project 0150315694502 iliyofunguliwa katika benki ya CRDB tawi la Mlimani City”,alisema Dk.Turuka.

Mradi huo uliozinduliwa na aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye kwa sasa ni Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 2009, tayari umekwisha fanyiwa majaribio mikoa ya Arusha na Dodoma ambapo ulionesha mafaniko makubwa.

Akizungumzia changamoto zinazowakabili, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Prof.John Nkoma alisema ni pamoja na uhaba wa fedha na baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu kuiba miundombinu ya anuwani hizo ikiwemo vibao vya kuonesha mitaa.

Nkoma alisema gharama za mradi huo mkubwa na unaoongeza ajira kupitia utalii, tayari umekwisha peleka kikosi kazi nchini Afrika Kusini ili kujifunza namna ya kuweka anuwani za makazi kwenye makazi yasiyopimwa.

Kwa upande wake Meya wa Jiji la Dar es salaam,Dk.Didas Masaburi alisema jiji lina zaidi ya 70% ya maeneo ambayo hayajapimwa jambo linalofanya kazi kuwa kubwa zaidi huku muda zaidi ukihitajika kutengwa ili kuhakikisha kila nyumba inapatiwa namba yake.

Wajumbe wengine ni wizara ya Miundombinu na Mawasiliano ya Zanzibar, Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati ya SMZ, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa-Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa pamoja na wizara ya Fedha.

Aidha,wajumbe wengine wa kamati hii ni viongozi wa juu wa taasisi zifuatazo.Mkurugenzi Mkuu TCRA,Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC),Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Vitambulisho vya Taida (NIDA) na Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

Prof.Nkoma pia aliwatoa wasiwasi wananchi kuwa anuwani hizo hazimzuii mtu yeyote kuhama kutoka eneo moja hadi jingine kutokana na kuwa na mfumo unaowezesha kubadilisha anuwani kama ilivyo kwa kadi za benki ambapo mteja huweza kubadilisha namba ya siri muda wowote apendapo.

No comments:

Post a Comment