Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, August 14, 2012

Waislamu waaswa kutafuta fadhila na rehma za Allah katika mwezi wa Ramadhaan


 Mufti Mkuu waZanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi akibadilishana mawazo na Makamu wa Kwanza waRais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad mara baada ya kuwasili nyumbani kwakeMbweni kwa ajili ya futari ya pamoja. Katikati ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar SheikhKhamis Haji
Baadhi ya viongoziwa Dini na Serikali pamoja na wananchi, wakijumuika pamoja katika futariiliyoandaliwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad, hukonyumbani kwake Mbweni. (picha na Salmin Said, OMKR).   

Na Hassan Hamad OMKR

Waislamu nchini wametakiwa kufarijiana ili kutafuta rehema za Mwenyezi Mungu zinazopatikana katika mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Wito huo umetolewa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi alipokuwa akizungumza na waislamu mbali mbali katika hafla ya futari iliyoandaliwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad huko nyumbani kwake Mbweni.

Amesema kufarijiana sio lazima kuwa na mali nyingi, bali ni kutoa kitu chochote kwa ajili ya MwenyeziMungu kwa lengo la kutafuta Rehema na Radhi zake.

“Hata ukitoa kokwa moja ya tende au chupa ya maji kwa mtu aliyefunga basi inatosha kuwa sadaka yako, nanaamini kila mmoja wetu anao uwezo huo, bali kitu cha msingi ni kuwa na nia thabiti”, alifahamisha Sheikh Kabi.


Amesema kitendo cha kufarijiana hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan kinazidisha umoja,m shikamano na mapenzi miongoni mwa waislamu, na kuwataka kuendeleza utamaduni huo ambao ni wa kihistoria kwa Zanzibar.

Amemshukuru Makamu waKwanza wa Rais kwa kuandaa futari hiyo iliyowakutanisha viongozi mbali mbali wa serikali na dini wakiwemo mawaziri, makatibu wakuu na viongozi kadhaa wa dini akiwemo Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji.

Sheikh Kabi ametumia fursa hiyo kuiombea nchi iendelee kuwa na amani na utulivu, sambamba na kuwaombea viongozi wa nchi na wazanzibari kwa ujumla, na kuwataka kuepukana na mifarakano isiyokuwa na maslahi kwa nchi.

“Wananchi sasa tunaishikwa amani baada ya miaka kadhaa ya mifarakano katika nchi yetu, tunataka amani hii iendelee na kamwe tusirudi tena huko tulikotoka”, alitanabahisha Sheikh Kabi.

Aidha Sheikh Kabi ametoa wito kwa  wazazi na walezi kuendeleza vitendo vyema ili kuvirithisha vizazi vyao mambo mazuri ambayo yatawasaidia duniani na akhera.

Kwa upande wake Makamuwa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amewashukuru viongozi hao kwa kuitikia wito wa kufutari pamoja, na kwamba amepata faraja kubwa kutokana na mwitiko huo.

Viongozi wengine walioshiriki kwenye futari hiyo ni pamoja na Katibu Mkuu kiongozi Dkt Abdulhamid Yahya Mzee, Waziri wa Katiba na Sheiria Mhe. Abubakar Khamis Bakari na mwanasiasa mkongwe wa Zanzibar Mzee Hassan Nassor Moyo.

No comments:

Post a Comment