Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, January 17, 2013

Wanamgambo Algeria wazima oparesheni ya jeshi




Kiwanda cha kusafisha gesi asilia walikotekwa nyara wageni Algeria
Wanamgambo nchini Algeria wanasema wamefanikiwa kuzima shambulizi la Jeshi la Algeria lililokuwa na lengo la kuwanusuru makumi ya raia wa kigeni waliotekwa nyara jana wakiwemo raia wa Ufaransa, Uingereza na Marekani.
Imearifiwa kuwa, Jumatano usiku wanajeshi wa Algeria walijaribu kuingia katika kiwanda cha kusafisha gesi asilia katika mji wa In Amenas mashariki mwa nchi hiyo ambako wanamgamabo hao wanawashikilia makumi ya raia wa kigeni.
Mapema jana Jumatano alfajiri wanamgambo 20 waliokuwa na silaha nzito nzito walishambulia basi ambalo lilikuwa limewabeba raia wa kigeni wafanyao kazi katika kiwanda cha gesi. Katika tukio hilo raia mmoja wa Uingereza na mwingine wa Ufaransa waliuawa na wengine 41 kutekwa nyara. Raia wengine wa kigeni waliotekwa nyara katika tukio hilo ni kutoka Ireland, Japan na Norway. Wanamgambo hao wanasema kwamba watawaachilia huru mateka hao salama salimini kwa sharti la Ufaransa kusitisha mashambulizi yake ya kijeshi nchini Mali.

No comments:

Post a Comment