Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 1, 2013

Waasi wa Seleka watakiwa kufanya mazungumzo



Waasi wa Seleka watakiwa kufanya mazungumzo
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ufaransa amewataka viongozi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na Muungano wa Waasi wa Seleka wahitimishe mapigano na kukaa katika meza ya mazungumzo. Laurent Fabius ametoa wito pia wa kuundwa serikali ya muungano katika nchi hiyo ya Afrika ya Kati. Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ufaransa amenukuliwa na mtandao wa Intaneti wa wizara hiyo akisema kwamba, kwa sasa kufanyika mazungumzo baina ya waasi wa Seleka na serikali ya Rais Francois Bozize wa nchi hiyo ndio njia bora kabisa ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo.
Waziri Fabius amewataka waasi na serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati kujiepusha na hatua yoyote ile hasa katika mji mkuu Bangui ambayo inakinzana na roho ya mazungumzo na amani katika nchi hiyo sambamba na kulinda usalama wa raia. Wakati huo huo, Waasi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wamekutana na Mwenyekiti wa  Umoja wa Afrika na kusema kuwa wako tayari kuchunguza pendekezo lililotolewa na Rais wa nchi hiyo la kushiriki katika serikali ya umoja wa kitaifa. Msemaji wa muungano wa waasi hao wa Seleka amesema kwamba, hata hivyo lengo lao si kuingia serikalini bali ni kuwawezesha wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati  kupata maendeleo na kujitegemea.

No comments:

Post a Comment