Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, January 18, 2013

Sudan Kusini yaanza kuondoka mpakani




Sudan Kusini yaanza kuondoka mpakaniSerikali ya Sudan Kusini imetangaza kuwa, imeanza kuondoa askari wake katika maeneo ya mpaka wake na Sudan, kwa ajili ya kuanzisha eneo huru kati ya nchi mbili hizo jirani. Ripoti iliyotolewa jana na serikali ya Juba ilibainisha kuwa, mwisho wa kuondoka vikosi vya nchi hiyo katika maeneo hayo ya mpakani ni tarehe 4 mwezi ujao wa Februari na kwamba, Sudan Kusini inatarajia kuona Khartoum nayo inachukua hatua mithili ya hiyo kama njia ya kutekeleza makubaliano yaliyotiwa saini na viongozi wa nchi mbili mjini Addis Abba, Ethiopia. Mwezi Septemba mwaka jana na chini ya mashinikizo ya kimataifa, Sudan na Sudan Kusini zilikubaliana kuondoa vikosi vyao katika maeneo yanayogombaniwa na pande mbili. Aidha viongozi wa nchi hizo Omar Hassan al-Bashir wa Sudan na Salva Kiir wa Sudan Kusini, walikubaliana kuanzisha eneo huru lisilo na askari wa upande wowote,
hatua iliyotajwa kuwa na lengo la kukata uungaji mkono kwa waasi wanaoendesha harakati zao katika maeneo ya mpakani.

No comments:

Post a Comment