Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, January 10, 2013

Wafanyakazi wa majumbani TZ wakabiliwa na matatizo


Wafanyakazi wa majumbani TZ wakabiliwa na matatizoWafanyakazi wa majumbani nchini Tanzania wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kuweza kuwakomboa dhidi ya matatizo yanayowakabili licha ya kwamba sheria za kazi zinawatambua. Hayo yamedokezwa na Ofisi ya Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa –ILO- nchini Tanzania. Mratibu wa mpango wa misaada ya maendeleo katika ofisi ya ILO nchini Tanzania, Anne-Marie Kiaga amesema changamoto hizo ni za pande tatu yaani usimamizi wa sheria, waajiriwa wenyewe pamoja na waajiri.
Bi. Kiaga amesema hata wakati huu ambapo ILO kwa kushirikiana na serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali inaendesha utafiti wa kina kufahamu idadi halisi ya wafanyakazi wa majumbani nchini Tanzania kuna changamoto wanazokumbana nazo ikiwemo kujitambua na hivyo kinachofanyika ni kuelimisha umma. Ripoti mpya ya shirika la Kazi duniani, ILO kuhusu hali ya wafanyakazi wa majumbani imeonyesha kupanuka kwa sekta hiyo huku mazingira ya kazi yakiendelea kuwa duni hususan katika nchi zinazoendelea. Ripoti hiyo imetoa mfano na kusema nchini Tanzania wastani wa saa za kazi kwa wafanyakazi wa majumbani kwa wiki ni saa 63 huku Austria ukiwa ni saa 15 kwa wiki, ilhali wastani huo unatakiwa uwe kati ya saa 40 na 48 kwa wiki.

No comments:

Post a Comment