Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 8, 2013

Mkutano wa Madhehebu za Kiislamu kufanyikaTehran


Ayatullah Mohsen Araki
Ayatullah Mohsen Araki
Mkutano wa Kukurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu unatarajiwa kufanyika hivi karibuni hapa mjini Tehran. Ayatullah Mohsen Araki Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kukurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu ambaye yuko safarini mjini London Uingereza amesema kuwa, mkutano huo utafanyika tarehe 28 na 29 za  mwezi huu wa Januari hapa mjini Tehran. Ayatullah Araki amesema kuwa, wageni kutoka nchi 100 duniani wanatarajiwa kushiriki katika mkutano huo. Ameongeza kuwa, mkutano huo utafuatilia mikakati na maazimio yaliyopasishwa katika mkutano uliopita. Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kukurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu ameashiria mwamko wa Kiislamu katika ulimwengu wa Kiarabu na kusema kuwa, Wamagharibi wanafanya njama za kuzusha fitina na mifarakano baina ya Waislamu hivyo Waislamu wanapaswa kuwa macho na njama hizo.

No comments:

Post a Comment