Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 1, 2013

Waandishi wa habari 121 waliuawa mwaka 2012


Waandishi wa habari 121 waliuawa mwaka 2012
Jim Boumelha Mkuu wa Muungano wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari amesema kuwa, jumla ya waandishi wa habari 121 waliuawa kwenye matukio mbalimbali yaliyojiri katika pembe zote za dunia mwaka 2012. Akitoa taarifa hiyo hapo jana nchini Ubelgiji, Boumelha amesema kuwa, waandishi hao wa habari waliuawa kwenye machafuko au matukio mbalimbali wakati wa kutekeleza majukumu yao ya kikazi.
Mkuu wa Muungano wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari amezitaka serikali zote ulimwenguni kuchukua hatua za kivitendo za kuzuia mauaji dhidi ya waandishi wa habari ambao amesema wana jukumu muhimu la kufichua na kueleza uhakika wa mambo na kuufikisha mbele ya fikra za walio wengi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jim Boumelha nchi za Somalia, Pakistan na Mexico zilikuwa hatari zaidi katika shughuli za waandishi wa habari mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment