Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 8, 2013

Jeshi la Israel lashambulia Ukingo wa Magharibi



Jeshi la Israel lashambulia Ukingo wa Magharibi Kwa mara nyingine askari wa utawala wa Kizayuni umefanya mashambulizi dhidi ya maeneo tofauti ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuwatia mbaroni Wapalestina wasiopungua 4. Duru za habari za Palestina zinaarifu kuwa, jana pia askari hao walivamia mji huo na kuwatia mbaroni Wapalestina 13 na kufanya idadi ya Wapalestina waliotiwa mbaroni ndani ya kipindi cha siku mbili kuwa 17. Hii ni katika hali ambayo, karibu kila siku askari hao huyavamia maeneo tofauti ya raia wa Palestina na kuwatia mbaroni raia hao wa maeneo hayo. Ni vyema kuashiria hapa kwamba, karibu Wapalestina elfu tano wanaendelea kuzuiliwa katika jela za utawala huo. Wakati huo huo Khalid Mash'al, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas na Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina wanatazamiwa kukutana hapo kesho mjini Cairo na kujadili kuhusiana na mazungumzo ya kitaifa yaliyokuwa yakisuasua kwa miaka mingi. Duru za habari zimearifu kuwa, tayari Khalid Mash'al amewasili leo mjini Cairo huku Abbas akitarajiwa kuwasili nchini humo hapo kesho kwa ajili ya mazungumzo hayo.

No comments:

Post a Comment