Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 29, 2013

Watu sita wauawa, Waziri Mkuu Somalia anusurika


Mwanajeshi wa serikali ya Somalia katika eneo la mlipuko wa huko nyuma mjini Mogadishu Mwanajeshi wa serikali ya Somalia katika eneo la mlipuko wa huko nyuma mjini Mogadishu
Watu wasiopungua sita wameuawa kufuatia mlipuko wa bomu nje kidogo ya ofisi ya Waziri Mkuu wa Somalia mjini Mogadishu.
Hujuma hiyo imejiri leo Jumanne mchana ambapo kati ya waliouawa ni maafisa wa usalama. Imearifiwa kuwa mtu aliyekuwa amejifunga mshipi wa bomu alijiripua karibu na ofiisi ya Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon katika eneo la kati kati mwa Mogadishu. Maafisa wa usalama wanasema waziri mkuu alikuwa ofisi wakati wa tukio hilo lakini hakujeruhiwa.

Hakuna kundi lolote lililodai kuhusika na mripuko huo lakini kundi la kigaidi la al-Shabab limeapa kuipundua serikali ya Somalia.

No comments:

Post a Comment