Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, January 10, 2013

Drone’ ya Marekani yaua watu wanne Pakistan



‘Drone’ ya Marekani yaua watu wanne Pakistan
Watu wanne wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa kufuatia hujuma ya ndege isiyo na rubani ya Marekani yaani Drone katika eneo la Waziristan Kaskazini nchini Pakistan.
Duru zinaarifu kuwa ndege hiyo imevurumisha makombora manne katika nyumba moja na kusababisha maafa na hasara mapema leo asubuhi.
Mara kwa mara ndege zisizo na rubani za Marekani hutekeleza mashambulizi katika maeneo kadhaa ya Pakistan kwa kisingizio cha kupambana na magaidi. Hata hivyo wahanga wakuu wa hujuma hizo za Marekani ni raia wakiwemo wanawake na watoto wasio na hatia.
Marekani inatekeleza hujuma za ndege zisizio na rubani katika nchi kadhaa za Kiislamu kama vile Afghanistan, Yemen na Somalia kwa kisingizio hicho hicho cha kupambana na ugaidi lakini wahanga wakuu huwa ni raia.

Wataalamu wa sheria za kimataifa wanasema hujuma hizo za ‘Drone’ ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.

No comments:

Post a Comment