Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 1, 2013

Kikwete: Hatua ya kwanza ya katiba mpya imekamilika


Kikwete: Hatua ya kwanza ya katiba mpya imekamilika
Rais Jakaya Kikwete wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, Tume ya Mabadiliko ya Katiba imekamilisha hatua ya kwanza ya kukusanya maoni ya mtu mmoja mmoja nchi nzima na kwamba, hatua inayofuata ni ya kukusanya maoni ya makundi maalumu. Akizungumza kwa mnasaba wa kuwadia mwaka mpya wa 2013 Miladia, Rais Kikwete amesema, Bunge la Katiba, litakaa Novemba mwaka huu kupitisha mapendekezo ya Katiba Mpya. Rais Kikwete amesisitiza kwamba, kama kila kitu kitakwenda kama inavyotarajiwa, Katiba Mpya iliyotokana na maoni na matakwa ya wananchi itapatikana ifikapo mwaka 2014.
Wakati huo huo, Rais Kikwete amewataka Watanzania kupanga uzazi na kueleza kwamba, matokeo ya sensa iliyofanyika mwezi Agosti mwaka huu yanaonesha kuwa, idadi ya Watanzania imefikia milioni 45 na hiyo ni ishara kwamba ifikapo mwaka 2016 kuna uwezekano wa idadi hiyo kufikia milioni 51 jambo ambalo linaweza kuwa ni mzigo kwa taifa, jamii na hata katika masuala ya uchumi.

No comments:

Post a Comment