Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, January 18, 2013

Tunisia yaonya kuathiri vibaya mgogoro wa Mali



Rais Muncef Marzouki wa Tunisia
Rais Muncef Marzouki wa TunisiaSerikali ya Tunisia imeonya kuhusiana na taathira mbaya zinazoweza kulikumba eneo zima la Sahel na nchi za magharibi mwa Bara Arabu kutokana na uingiliaji kijeshi nchini Mali. Hayo yalisemwa jana na Rais Moncef Marzouki wa Tunisia ambaye amesisitizia pia udharura wa kuimarishwa mawasiliano na mshikamano kwa ajili ya kuitafutia ufumbuzi kadhia ya Mali. Katika ripoti hiyo iliyotolewa baada ya kikao cha mawaziri wa ulinzi na wa mambo ya nje wa nchi hiyo, imeelezwa kwamba,
mgogoro unaoendelea hivi sasa nchini Mali ni hatari kubwa kwa nchi jirani ikiwemo Tunisia. Aidha ripoti hiyo imesisitiza kuwa, Tunisia inaunga mkono umoja na amani wa taifa la Mali dhidi ya makundi ya kigaidi. Aidha mawaziri wa Tunisia walilaani vitendo vya utekaji nyara vilivyofanywa na makundi ya kigaidi huko kusini mwa Algeria na kutangaza kuwa Tunisia iko pamoja na serikali ya Algiers dhidi vitendo hivyo.

No comments:

Post a Comment