Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 1, 2013

Mai Mai walia na mazungumzo Congo


Mai Mai walia na mazungumzo Congo Wanamgambo wa Mai Mai katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametoa wito wa kujumuishwa katika mazungumzo ya amani baina ya serikali na waasi wa M23. Joseph Assanda mmoja wa viongozi wa wanamgambo wa Mai Mai katika Jimbo la Kivu Kusini amesema kuwa, kundi lao linapaswa kujumuishwa katika mazungumzo ya amani baina ya serikali na M23. Hayo yanajiri katika hali ambayo, mazungumzo ya waasi wa M23 na serikali ya Kinshasa yaliyokuwa yakifanyika mjini Kampala Uganda, yameendelea kukosolewa na wapinzani ambao wanataka makundi mengine ya upinzani yajumuishwe katika mazungumzo hayo. Wakati huo huo,
mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Kinshasa na waasi hao yanatarajiwa kuendelea tena mwezi huu wa Januari baada ya kumalizika sherehe za Krismasi na mwaka mpya. Tangu Mei mwaka jana zaidi ya watu laki tisa wamelazimika kuyakimbia makazi yao mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufuatia machafuko na ukosefu wa usalama katika maeneo hayo. Baadhi ya raia hao wamelazimika kukimbilia katika nchi jirani za Rwanda na Uganda.

No comments:

Post a Comment