Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, January 22, 2013

Utulivu warejea Eritrea baada ya uasi jeshini


Rais Issaias Afeworki wa EritreaSerikali ya Eritrea imesema kuwa, hali katika mji mkuu Asmara ni tulivu baada ya kushindwa nguvu wanajeshi waasi waliokuwa wamechukua udhibiti wa jengo la Wizara ya Habari.
Yemane Gebremeskel, mkurugenzi wa ofisi ya Rais Issaias Afeworki wa Eritrea amethibitisha kutulia hali ya mambo.
Kundi moja la askari waasi katika Jeshi la Eritrea walizingira Wizara ya Habari Jumatatu na kulazimisha Shirika la Utangazaji la Taifa kutangaza kuachiliwa huru wafungwa wote wa kisiasa.
Wanajeshi hao waasi walimlazimisha mkuu wa televisheni ya serikali kusoma tangazo hilo.

Kwa kawaida huwa vigumu kuthibitisha habari kutoka Eritrea kwani hakuna chombo chochote cha habari cha kigeni nchini humo.
Duru za wapinzani zinasema kuwa, wanajeshi hao waasi wapatao 100 walisalimu amri baada ya serikali kusema itatelekeza matakwa yao. Mwaka jana Umoja wa Mataifa ulikadiria kuwa, kuna kati ya wafunwa elfu tano hadi elfu kumi wa kisiasa nchini Eritrea.

No comments:

Post a Comment