
huku baadhi ya vyombo vya kupasha habari na hata taasisi na asasi za kiserikali za Marekani zikishajiisha vitendo hivyo vilivyo dhidi ya ubinadamu. Nadhira al Khalili Wakili na Mshauri wa Masuala ya Kisheria wa Baraza la Uhusiano wa Marekani na Uislamu amesema kuwa, kanali za televisheni kama vile Fox News mara nyingi huwaarifisha Waislamu kuwa magaidi, na kuwapotosha watu walio na uelewa mdogo. Wakili Nadhira ameongeza kuwa, baadhi ya washambuliaji wamekiri kwenye vituo vya polisi kuwa wamewashambulia Masingasinga na Wahindu wakidhani kwamba ni Waislamu. Al Khalili ameongeza kuwa, Waislamu mithili ya watu wengine ni watu wenye kupenda amani na utulivu nchini humo.
No comments:
Post a Comment