skip to main |
skip to sidebar
Shughuli za kukusanya maoni ya katiba TZ zachafuka
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania
amejikuta mashakani baada ya kutoa agizo la kupinga kutolewa baadhi ya
maoni na wananchi. Jaji Mustaafu Joseph Warioba anayeongoza tume hiyo
yenye dhima ya kukusanya maoni kuhusu katiba mpya ameagiza maafisa
kutopokea maoni ya makundi maalumu. Warioba amesema watu watoe maoni yao
binafsi bila kufungamana na makundi yoyote. Hatua hiyo imemuweka pabaya
jaji huyo mustaafu baada ya makundi ya kutetea haki za binadamu kusema
kuwa, agizo hilo ni ukiukaji wa haki ya kujieleza.
Huku hayo yakijiri
watumishi wa umma wamepata fursa ya kutoa maoni yao kuhusu katiba mpya.
Miongoni mwa mambo yaliyotawala kikao chao na maafisa wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba ni suala la mishahara bora pamoja na kuboreshwa
mazingira yao ya kazi. Tume hiyo inatarajiwa kumaliza kazi zake mwezi
Mei mwaka huu na kisha kura ya maoni kuitishwa baadaye.
Na: Salim Swaleh
No comments:
Post a Comment