Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, January 10, 2013

Rais Farole wa Puntland ajiongezea muhula


Rais Farole wa Puntland ajiongezea muhula
Rais wa eneo la Puntland lenye mamlaka ya ndani kaskazini mashariki mwa Somalia amejiongezea muda wa kutawala hadi Januari mwaka ujao wa 2014.
Akizungumza mjini Bodsaso, Rais Abdulrahman Mohammad Farole wa Puntland amesema ataendelea kutawala baada ya muhula wake kumalizika mwezi huu.
Farole amesema katiba inamruhusu kuongeza muhula wake kwa muda wa mwaka mmoja.
Wapinzani wanamlaumu rais huyo wa Puntland kuwa amekiuka sheria.
Eneo la Puntland lilijitangazia mamlaka ya ndani mwaka 1998 na limekuwa likishuhudia amani pamoja na kuwepo vita katika maeneo ya kati na kusini mwa Somalia.
Eneo la Somaliland lililoko kaskazini mwa Somalia tayari limeshajitangazia uhuru kamili ingawa bado halijatambuliwa na Umoja wa Mataifa.

No comments:

Post a Comment