Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, January 18, 2013

25 wauawa katika miripuko ya mabomu Iraq



25 wauawa katika miripuko ya mabomu Iraq
Duru za habari kutoka nchini Iraq zimearifu kuwa, zaidi ya watu 25 wameripotiwa kuuawa katika maeneo tofauti nchini humo. Habari zinasema kuwa, mauaji hayo yalitokea jana katika mfululizo wa miripuko ya mabomu iliyotokea katika maeneo tofauti nchini Iraq. Mauaji hayo yanajiri baada ya mfululizo wa mauaji yaliyosababishwa na mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea katika siku tatu zilizopita kwenye maeneo kadhaa ya nchi hiyo, na kupelekea kuuawa zaidi ya watu 81 na kujeruhiwa mamia ya wengine. Hadi sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na mauaji hayo. Viongozi wa Iraq wamekuwa wakizituhumu nchi za Saudia na Qatar kuwa, zinayaunga mkono makundi ya kigaidi yanayofanya mauaji nchini humo, kama njia ya kutekeleza siasa za Marekani kwenye eneo la Mashariki ya Kati. Wakati huo huo serikali ya Baghdad imetangaza kuwa, polisi ya nchi hiyo imefanikiwa kuwaangamiza magaidi 10 katika mkoa wa Al-Anbar nchini humo.

No comments:

Post a Comment