Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, January 10, 2013

Mapigano makali yajiri katikati mwa Mali

Mapigano makali yajiri katikati mwa Mali
Wanajeshi wa Mali wamepambana vikali na wanamgambo wanaokalia eneo la kaskazini katika mji wa Konna ulioko katika eneo la katikati mwa nchi hiyo.
Wakaazi wa Konna wanasema siku ya Jumatano kulikuwa na ufyatulianaji risasi wa masaa kadhaa kati ya waasi na wanajeshi wa serikali.
Mapigano hayo yamejiri masaa 48 baada ya vikosi vya serikali kujaribu kuudhibti mji huo.
Duru mpya ya mashambulizi ya waasi inajiri baada ya mazungumzo ya amani kati ya pande hasimu kuakhirishwa. Mazungumzo hayo yalikuwa yaanze leo katika mji mkuu wa Burkina Faso, Ouagadougou.

Kabla ya hapo kulitangazwa kuwepo maandalizi ya waasi wanaofungamana na kundi la Ansarud-Din na Harakati ya Umoja na Jihad katika eneo la Magharibi mwa Afrika, kwa ajili ya kufanya mazungumzo na serikali ya Bamako ili kuupatia ufumbuzi mgogoro unaoendelea kutokota nchini humo.

No comments:

Post a Comment