Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, January 10, 2013

Mshukiwa wa mauaji Rwanda awakataa majaji



Mshukiwa wa mauaji Rwanda awakataa majaji
Mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Leon Mugesera amefungua kesi akitaka majaji wawili kati ya watatu wanaosikiliza kesi yake waondolewe.
Mugesera alifikishwa kizimbani katika Mahakama Kuu ya Rwanda lakini punde baada ya kuwasili hapo alifungua kesi akitaka majaji Athanase Bakuzakundi na Eugene Ndagijimana wazuiwe kusikiliza kesi yake. Amesema kwa mujibu wa sheria ya taratibu za mahakama, majaji hao hawana haki ya kusikiliza kesi yake kwani waliwahi kusikiliza kesi zake ambazo alishindwa.
Mahakama inatazamiwa kutoa uamuzi wake leo Alkhamisi kuhusu pingamizi hiyo ya Mugesera ambaye alirejeshwa Rwanda kutoka katika maficho yake nchini Canada.
Mugesera anakabiliwa na mashtaka ya kushiriki katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda.

No comments:

Post a Comment