Rwanda imekataa kutoa viza kwa
maafisa wawili wa timu ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa iliyoituhumu
Kigali mwaka jana kuwa inawapa silaha waasi wa mashariki mwa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo na kuwataja kuwa watu wenye upendeleo.
Friday, March 29, 2013
Monday, March 25, 2013
Uamsho haina account wala page facebook
Masoud Khamis Al-Bimani
Jumuia ya UAMSHO na Mihadhara ya Kiislam Zanzibar haina account wala
page ya Facebook, lakini kuna watu kwa makusudi wameamua kutengeneza
Page ya Uamsho hapa FB, kwa lengo la kuitia Doa jumuiya, anakua anapost
vitu visivyo na Maana, kwa lengo la kuupotosha Umma tujihadhari na watu
hawa.
Kesi ya Uamsho yasomwa upya, yapangiwa Jaji Fatma
KESI ya jinai inayowakabili viongozi wa Dini wa Jumuiya ya Uwamsho na
Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) imeanza kusomwa upya leo katika Mahakama Kuu ya Zanzibar baada ya maamuzi ya awali kutenguliwa.
Kesi hiyo namba 9 ya mwaka 2012 ilisomwa mbele ya Jaji Fatma Hamid
Mahmoud na Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ramadhan Nassib, ambae
aliwataja washitakiwa hao kuwa ni Farid Hadi Ahmed (41) mkaazi wa Mbuyuni,
Wednesday, March 20, 2013
Al Qaeda wamuua mateka wa Kifaransa
Mtandao wa al Qaeda wa kaskazini mwa
Afrika umetangaza kuwa umemuua mateka wa Kifaransa katika kulipiza
kisasi uingiliaji wa kijeshi wa Ufaransa nchini Mali. Mateka huyo wa
Kifaransa kwa jina la Phillippe Verdon alikatwa kichwa na mtandao huo wa
al Qaida tarehe kumi mwezi huu katika kile kundi hilo lilichokisema
kuwa ni kulipiza kisasi cha mashambulizi yaliyoanzishwa na Paris huko
Mali. Verdon alikuwa mmoja kati ya raia wawili wa Ufaransa waliotekwa
nyara mwezi Novemba mwaka juzi huko kaskazini mwa Mali katika mji wa
Hombori.
Polisi ya Misri yamtia mbaroni binamu wa Gaddafi
Polisi ya Misri imesema kuwa imemtia
mbaroni binamu na aliyekuwa mpambe wa karibu wa Muammar Gaddafi
kiongozi wa zamani wa Libya. Hapo jana maafisa wa Misri walisema kuwa
Ahmed Gaddaf al Dam alitiwa nguvuni baada ya vikosi vya usalama
kuizingira nyumba yake katika kitongoji cha Zamalek huko Cairo. Afisa
mmoja wa Misri amesema kuwa afisa huyo wa zamani wa intelijinsia wa
utawala wa Gaddafi atakabidhiwa kwa maafisa wa Libya hivi karibuni.
Baada ya kuzingirwa nyumba yake kwa masaa kadhaa huko katikati mwa
Cairo, binamu huyo wa Muammar Gaddafi alisikika akizungumza na kanali
moja ya televisheni kwa njia ya simu na hapa ninamnukuu" tulifika hapa
kwa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri na baraza la kijeshi,
sisi si magaidi wa kuweza kushambuliwa namna hii," mwisho wa kumnukuu.
Tuesday, March 19, 2013
37 wafariki dunia katika ajali ya basi India

Polisi ya India imeeleza kuwa, ajali hiyo mbaya imetokea mapema leo alfajiri katika wilaya ya Maharashtra. Polisi ya Usalama barabarani nchini India imeeleza kuwa, basi hilo lilikuwa likitokea katika mji wa Goa na kuelekea Mumbai; na kwamba dereva wa basi hilo alishindwa kulidhibiti na kutumbukia mtoni. Polisi imeeleza kuwa, ajali hiyo imetokea umbali wa kilomita 350 kusini mwa Mumbai.
Polisi imeeleza kuwa, watu wasiopungua 17 wamejeruhiwa akiwemo dereva wa basi hilo, ambaye hali yake imeelezwa kuwa ni mahututi. Taarifa za awali zinasema kuwa, ndani ya basi hilo kulikuwa na idadi kadhaa ya watalii kutoka nje ya nchi hiyo.
Siasa za Wamagharibi ni za kindumakuwili
Katibu Mkuu wa Harakati ya Ukombozi ya Bahrain amezikosoa vikali
siasa za kindumakuwili za Magharibi kuhusiana na matukio ya kieneo na
ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Bahrain unaofanywa na
utawala wa Aal Khalifa wa nchi hiyo.
Saeed al Shahabi ameongozana na maelfu ya wapinzani wa Bahrain na kukusanyika mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza mjini London na kusema kuwa, uungaji mkono wa kibubusa wa Marekani na Uingereza kwa utawala wa Aal Khalifa umesababisha utawala huo kuvimba kichwa na kupuuza misingi ya haki za binadamu.
Ameongeza kuwa, siasa za kindumakuwili za nchi za Magharibi sio za kikhlaki na amebainisha kuwa, Washington na London zinapaswa kukomesha uungaji mkono wao kwa utawala wa Bahrain ambao unatenda jinai za mauaji, kuwafunga na kuwashikilia korokoroni wanaharakati na kuwatesa wananchi wa nchi hiyo wanaume na wanawake.
Saeed al Shahabi ameongozana na maelfu ya wapinzani wa Bahrain na kukusanyika mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza mjini London na kusema kuwa, uungaji mkono wa kibubusa wa Marekani na Uingereza kwa utawala wa Aal Khalifa umesababisha utawala huo kuvimba kichwa na kupuuza misingi ya haki za binadamu.
Ameongeza kuwa, siasa za kindumakuwili za nchi za Magharibi sio za kikhlaki na amebainisha kuwa, Washington na London zinapaswa kukomesha uungaji mkono wao kwa utawala wa Bahrain ambao unatenda jinai za mauaji, kuwafunga na kuwashikilia korokoroni wanaharakati na kuwatesa wananchi wa nchi hiyo wanaume na wanawake.
Boko Haram waua walimu watatu Nigeria

Wazimbabwe waipigia kura ya ndio katiba mpya
Matokeo yasiyo rasmi ya kura ya maoni ya katiba mpya nchini
Zimbabwe, yanaonyesha kwamba, wananchi wameipigia kura ya ndio katiba
hiyo ambayo inapunguza madaraka ya rais wa baadaye wa nchi hiyo. Ripoti
zilizosambazwa leo kutoka vituo vya kuhesabu kura, zinaonyesha kuwa,
watu milioni tatu na laki moja kati ya watu milioni tatu na laki nne
waliofika kwenye vituo vya kupigia kura nchini humo, wameipigia kura ya
ndio katiba mpya ya nchi hiyo ya kusini mwa Afrika inayokabiliwa na
mgogoro mkubwa wa kiuchumi. Gazeti la Herald limeripoti kuwa, watu laki
mbili wameipigia kura ya hapana katiba hiyo. Kwa mujibu wa takwimu rasmi
za nchi hiyo, Wazimbabwe milioni sita pekee ndio waliokamilisha
masharti ya kupiga kura nchini. Ilitarajiwa kuwa, hadi kufikia jioni ya
leo, Tume ya Uchaguzi nchini humo ingekuwa imekamilisha kazi za kuhesabu
kura na kutangaza matokeo rasmi ya kura hiyo.
Mapigano kati ya jeshi na waasi Sudan Kusini

Monday, March 18, 2013
Watu 10 wauawa kwenye mlipuko nchini Somalia
Habari kutoka Mogadishu, mji mkuu wa Somalia zinasema kuwa, kwa
akali watu 10 wamefariki dunia na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia
mlipuko mkubwa wa bomu uliotokea karibu na ukumbi wa kitaifa wa michezo
ya kuigiza.
Habari zaidi zinasema kuwa, bomu hilo lilikuwa limetegwa kwenye gari na kwamba Mkuu wa Usalama wa Mogadishu ndiye alikuwa mlengwa mkuu. Haijabainika wazi iwapo mkuu huyo ameuawa au la.
Kundi la wanamgambo la Al-shabab tayari limedai kuhusika na shambulio hilo. Kundi hilo limeapa kumuondoa madarakani Rais Hassan Sheikh Mohamud, aliyechaguliwa na bunge la Somalia mwaka uliopita. Hii ni katika hali ambayo, wanamgambo hao wanaripotiwa kuuteka mji wa Hudur wa kusini mwa Somalia.
Habari zaidi zinasema kuwa, bomu hilo lilikuwa limetegwa kwenye gari na kwamba Mkuu wa Usalama wa Mogadishu ndiye alikuwa mlengwa mkuu. Haijabainika wazi iwapo mkuu huyo ameuawa au la.
Kundi la wanamgambo la Al-shabab tayari limedai kuhusika na shambulio hilo. Kundi hilo limeapa kumuondoa madarakani Rais Hassan Sheikh Mohamud, aliyechaguliwa na bunge la Somalia mwaka uliopita. Hii ni katika hali ambayo, wanamgambo hao wanaripotiwa kuuteka mji wa Hudur wa kusini mwa Somalia.
Wayemen waanza mazungumzo ya kitaifa

Mazungumzo hayo yamefunguliwa na Rais Abdrabuh Mansur Hadi wa nchi hiyo na yanahudhuriwa na zaidi ya wawakilishi 500 kutoka vyama vya kisiasa vya Yemen. Hata hivyo mrengo wa kisiasa wa kusini umesusia mazungumzo hayo na uliitisha maandamano na mgomo katika mji wa Aden hapo jana kupinga suala hilo.
Benki ya Dunia yazisaidia Msumbiji, Malawi na Zambia

Hayo yameelezwa na Tijan Sallah Meneja wa Sekta ya Kilimo na Umwagiliaji katika ukanda huo. Sallah ameongeza kuwa lengo la kutekelezwa mpango huo ni kuboresha sekta ya kilimo katika nchi hizo za Kiafrika. Amesema kuwa, Benki ya Dunia imeamua kutoa misaada yake kwa nchi hizo kwa lengo la kustawisha zaidi utafiti katika sekta ya kilimo na kuboresha mafunzo kwenye sekta hiyo.
Hatari zilizosalia baada ya kukaliwa kwa mabavu Iraq

Wataalamu wa mambo na mashirika ya afya ya Iraq yametahadharisha kuhusu hatari za athari mbaya za uvamizi na kukaliwa kwa mabavu Iraq na vikosi vya Marekani na kueleza kuwa Marekani ilitumia tani 35 za urani katika vita huko Iraq suala linalotishia maisha ya vizazi vijavyo. Munthi Mahmoud Shukr mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Baghdad ameashiria athari haribifu za urani kwa raia na mazingira ya maeneo yaliyoathiriwa na kueleza kuwa Marekani iliwatumia raia wa Iraq kama mapanya wa maabara na majaribio yake mbalimbali.
Wafungwa wa Guantanamo waendelea kugoma kula
Mgomo wa kula chakula unaoendelea kufanywa na wafungwa walioko
katika jela ya Guantanamo umeingia katika siku ya 41 huku wataalamu wa
kitiba na mawakili wanaowatetea wafungwa hao wakionya kuhusu kudhoofika
kiafya kwa wafungwa zaidi ya 100 waliogoma kula chakula. Mawakili na
maafisa wa tiba wameeleza kuwa wana wasiwasi na hali mbaya ya kiafya ya
wafungwa hao walioanza kugoma kula chakula tangu Februari 6 mwaka huu
baada ya wafanyakazi wa jela ya Guantanamo kupora vitu vya wafungwa hao
zikiwemo barua, picha na nakala za kitabu kitukufu cha Qu'rani wakati
walipozikagua seli zao.
Saturday, March 16, 2013
Charity School Bwejuu
The school offers compulsory education for orphans and for students coming from poor or dysfunctional families at no cost, but if possible, the families of the students are required to contribute a small amount towards the running cost of the school.
The school welcomes individuals, institutions or government departments to unconditionally support the school in order to achieve our goals. We are grateful to all our sponsors for their financial assistance, which is much needed for providing study materials like books and pens for our students, to finance the running cost of the school and the school's kitchen, pay salaries, upgrade the teachers' educational levels, establish a library and a laboratory, for our hostel and for adding further classes.
The Charity School Bwejuu also receives youth volunteer coaching from all over the world for three months or more. The school provides free lodging for the volunteers on the school grounds.
We welcome individuals and companies to sponsor a student for USD $374 per year or to sponsor a teacher for the school.
CHARITY SCHOOL BWEJUU
P.O. Box 1609,
Zanzibar, Tanzania.
Contact Number: +255777438075
Email: bwejuucharityschool@hotmmail.com
bwejuucharityschool@gmail.com Bank Details:
Account Number: 021- 0000215
Bank Name: Tanzania Postal Bank, Zanzibar Branch
Country:Tanzania
IF YOU NEED TO SEND TO US DOLLAR OUT OF TANZANIA.
TAPBTZTZ 36144524 CITY BANK N.A
111 WALL STREET 99, FLOW 19
New York /10043
Swift code: CITIVS 33
P.O. Box 1609,
Zanzibar, Tanzania.
Contact Number: +255777438075
Email: bwejuucharityschool@hotmmail.com
bwejuucharityschool@gmail.com Bank Details:
Account Number: 021- 0000215
Bank Name: Tanzania Postal Bank, Zanzibar Branch
Country:Tanzania
IF YOU NEED TO SEND TO US DOLLAR OUT OF TANZANIA.
TAPBTZTZ 36144524 CITY BANK N.A
111 WALL STREET 99, FLOW 19
New York /10043
Swift code: CITIVS 33
Friday, March 15, 2013
Mabadiliko ya tabia ya nchi, chanzo cha njaa Somalia
Utafiti unaonyesha kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi yanayotokana
na shughuli za kibinaadamu ni kati ya sabau za kutonyesha mvua za
kutosha Afrika Mashariki mwaka 2011 na hivyo ongezeko la joto duniani
limetajwa kuwa chanzo cha njaa nchini Somalia.
Hii ni mara ya kwanza kwa mabadiliko ya tabia ya nchi (climate change) kutajwa kuwa moja ya sababu za kuwepo janga la njaa. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Idara ya Hali ya Hewa Uingereza kuhusu mwenendo wa hali ya hewa Somalia mwaka 2010 na 2011, msimu wa mvua fupi ulifeli mwishoni mwa mwaka 2010 kutokana na sababu za kimaumbile za tukio la La Nina. Lakini sababu ya ukosefu wa mvua za masika mapema mwaka 2011 ilikuwa ni ongezeko la joto duniani,
Hii ni mara ya kwanza kwa mabadiliko ya tabia ya nchi (climate change) kutajwa kuwa moja ya sababu za kuwepo janga la njaa. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Idara ya Hali ya Hewa Uingereza kuhusu mwenendo wa hali ya hewa Somalia mwaka 2010 na 2011, msimu wa mvua fupi ulifeli mwishoni mwa mwaka 2010 kutokana na sababu za kimaumbile za tukio la La Nina. Lakini sababu ya ukosefu wa mvua za masika mapema mwaka 2011 ilikuwa ni ongezeko la joto duniani,
Nyama ya ng'ombe yachanganywa na ya nguruwe Norway
Maafisa wa kitengo cha kusimamia na kukagua bidhaa nchini Norway
wamegundua kuwepo kwa nyama ya nguruwe iliyochanganywa na nyama halali
nchini humo. Catherine Signe Svinland Mshauri wa Kitengo cha kusimamia
na kukagua bidhaa nchini Norway amesema kuwa, kimegunduliwa kiasi cha
asilimia 5 hadi 30 ya nyama ya ngurume kwenye nyama ya ng'ombe ambayo
imeandikwa kuwa halali kwenye maduka kadhaa nchini humo. Amesisitiza
kuwa kiwango hicho cha nyama ya nguruwe hakikuwekwa kwa bahati mbaya
kwenye nyama halali. Amesema kuwa, wakaguzi hao pia wamegundua kwenye
sehemu inayouzwa Pizza kukiwa na nyama ya ng'ombe lakini imechanganywa
kwa asilimia 60 na nyama ya nguruwe.
Sunday, March 10, 2013
Wanamisri watakiwa kuheshimu katiba ya nchi
Msemaji wa serikali ya Misri amesisitiza udharura wa kuheshimiwa
katiba ya nchi hiyo. Alaa al Hadidi msemaji wa Waziri Mkuu wa Misri
sambamba na kusisitiza udharura wa watu wote kuheshimu sheria na katiba
ya nchi hiyo amewataka Wamisri, kutanguliza mbele maslahi ya kitaifa
kuliko ya makundi yao binafsi na kujiepusha kuharibu miundombinu na
majengo nchini humo. Al Hadidi amesema, haki ya kujieleza na kuandamana
kwa amani nchini Misri inapaswa kuheshimiwa lakini wakati huo huo
ameyataka makundi yote ya nchi hiyo kuacha kuharibu miundombinu na
kuchoma moto majengo ya serikali na yasiyokuwa ya serikali.
Kwa siku kadhaa miji tofauti ya Misri imeshuhudia vurugu na makabiliano kati ya wanaounga mkono serikali na wanaoipinga, huku baadhi ya vikundi vikichoma moto maeneo ya umma na majengo ya serikali.
Kwa siku kadhaa miji tofauti ya Misri imeshuhudia vurugu na makabiliano kati ya wanaounga mkono serikali na wanaoipinga, huku baadhi ya vikundi vikichoma moto maeneo ya umma na majengo ya serikali.
Wanajeshi wa DRC walionajisi wanawake kukamatwa

Akizungumza na waandishi habari mjini Kinshasa siku ya Jumamosi, Ntambo amesema wizara yake haitavumilia utovu wa nidhamu jeshini na kwamba wanajeshi wanaohusika na vitendo vya uhalifu watachukuliwa hatua kali.
Alkhamisi iliyopita kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo MONUSCO kilitishia kutoshirikiana na batalioni mbili za jeshi la nchi hiyo hadi pale watakapofikishwa mahakamani wanajeshi wanaotuhumiwa kuhusika na kunajisi wanawake mashariki mwa nchi hiyo.
Afisa mwandamizi wa Umoja wa Mataifa ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema batalioni hizo mbili zimetakiwa kuwafungulia mashtaka askari waliowanajisi wanawake katika mji wa Minova.
Uhuru Kenyatta achaguliwa kuwa rais wa Kenya

Kwa mujibu wa matokeo ya
uchaguzi wa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta mgombea wa kiti cha urais kwa
tiketi ya Muungano Jubilee ameshinda uchaguzi huo katika mchuano mkali
na mpinzani wake Raila Odinga wa mrengo wa Cord. Uhuru Kenyatta amepata
asilimia 50.07 na mpinzani wake wa karibu yaani Waziri Mkuu Raila Odinga
amepata asilimia 43.28 ya kura zote.
Uhuru ni mwana wa Jomo
Kenyatta shujaa wa ukombozi wa Kenya, na sasa anashika hatamu za
kuongoza Kenya baada miaka 50 tangu nchi hiyo ipate uhuru. Uhuru
Kenyatta ameweza kumshinda mpinzani wake mkuu Raila Odinga kwa kumpita
kwa kura laki nane katika uchaguzi wa rais uliofanyika tarehe 4 mwezi
huu. Mchuano mkali uliokuwepo kati ya wagombea hao wawili uliwafanya
weledi wa mambo watabiri uwezekano wa uchaguzi huo kuingia katika duru
ya pili hapo tarehe 11 mwezi Aprili.
Saturday, March 9, 2013
Kamanda wa Kutuliza Ghasia Misri atimuliwa kazi
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri amemtimua kazi Meja Jenerali
Majid Nouh Kamanda wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia nchini humo. Meja
Jenerali Muhammad Ibrahim al Juma'a amemtimua kazi Meja Jenerali Majid
Nouh na badala yake amemteua Meja Jenerali Ashraf Abdullah kuziba nafasi
hiyo. Siku ya Alhamisi iliyopita, mamia ya polisi wa Misri walifanya
mgomo na kutaka aondolewe Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo.
Polisi wa Misri wanamtuhumu waziri huyo kuwa alitumia kikosi cha
usalama kwa shabaha ya kufikia malengo yake ya kisiasa. Kwa upande
mwengine, jeshi la polisi katika mji wa Port Said nchini Misri
limekabidhi ulinzi wa usalama wa mji huo kwa jeshi la nchi hiyo ili
kukabiliana na ghasia na machafuko ya barabarani yanayoendelea mjini
humo kwa siku kadhaa sasa.
Mamilioni walalamikia marufuku ya hijabu Uturuki
Zaidi ya watu milioni 12 wametaka iondoshwe marufuku ya hijabu
nchini Uturuki. Mkuu wa Vyama vya Wafanyakazi Serikalini nchini
Uturuki amesema kuwa, jumla ya watu milioni 12 wanapinga kuendelezwa
marufuku ya hijabu mashuleni na hata kunyimwa ajira wanawake wanaovaa
hijabu kwenye sekta za serikali nchini humo. Mkuu wa Vyama vya
Wafanyakazi Serikalini nchini Uturuki amewasilisha ombi hilo kwa Waziri
wa Kazi na Ustawi wa Jamii wa Uturuki jumla ya saini za watu milioni 12
wanaotaka kuondoshwa marufuku ya hijabu nchini humo. Waziri wa Kazi na
Ustawi wa Jamii wa Uturuki ameahidi kulipeleka ombi hilo mbele ya kikao
cha baraza la mawaziri nchini humo ili lijadiliwe upya.
Yemen yaiomba radhi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Vikosi vya usalama Bahrain vyawatesa wanawake
Kanali ya Televisheni ya al Manar ya nchini Lebanon imeripoti
kuwa, wanawake 11 wameuawa shahidi katika harakati za mapinduzi ya
wananchi wa Bahrain, na wengine 230 wanakabiliwa na mateso na
ukandamizaji mkubwa kwenye jela za kuogofya za utawala wa Aal Khalifa
nchini humo. Wakati ulimwengu ukiadhimisha siku ya tarehe 8 Machi ya
kila mwaka kuwa ni siku ya Wanawake Duniani, wanawake wa Bahrain
wanakabiliwa na hali ngumu ya kimaisha na kukiukwa haki zao nchini
humo. Taasisi ya Kutetea Haki za Binadamu nchini Bahrain imeeleza kuwa,
mara baada ya kuanza harakati za kimapinduzi nchini humo mwezi Februari
mwaka 2011,
Thursday, March 7, 2013
Berlusconi asukumwa jela mwaka 1 nchini Italia

Macky Sall ataka Madrasa za Kiislamu kuboreshwa

CORD yataka zoezi la kuhesabu kura lisimamishwe

Somalia: Waasi watakaojisalimisha wataingia jeshini
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amesema yuko tayari
kuwajumuisha wanachama wa kundi la Al-shabab katika jeshi la taifa iwapo
wataamua kuweka silaha chini na kujisalimisha kwa serikali. Rais Hassan
amesema nchi inamhitaji kila Msomali ili iweze kusimama wima na
kujiunga tena na nchi zingine za dunia. Kiongozi huyo pia amelishukuru
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kuiondolea nchi yake vikwazo
vya silaha kwa kipindi cha mwaka mmoja. Amesema fursa hiyo itaiwezesha
Mogadishu kujiimarisha zaidi kiusalama. Rais Hassan pia amezungumzia
hali ya taasisi muhimu nchini Somalia na kusema kuwa baadhi ya taasisi
kama vile idara ya mahakama ni dhaifu na ameitaka jamii ya kimataifa
kusaidia kuinua hadhi ya taasisi hizo.
'US, Israel zapanga kuteka maeneo ya mafuta Sudan'

Kwa mujibu wa Shirika la
Habari la Fars, chama hicho tawala nchini Sudan kimesema majasusi wa
Israel na Marekani wanaunga mkono makundi ya waasi hasa kundi la JEM la
Darfur. Chama cha Kongresi ya Taifa kimesema pamoja na kuwepo oparesheni
hizo za majasusi wa Kizayuni na Marekani,
Tuesday, March 5, 2013
Kiongozi Muadhamu: Uislamu unahimiza kupanda miti

Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei ameyasema hayo Jumanne mjini Tehran kwa mnasaba wa ‘Wiki ya Mazingira na Kupanda Miti’. Baada ya kupanda miche miwili, Kiongozi Muadhamu amesema kuwa kulinda miti na kuzuia uharibifu wa miti ni kati ya mambo yaliyosisitizwa katika dini tukufu ya Kiislamu.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuhusu udharura wa kuwepo azma na irada imara ya kuzuia unyakuzi wa maeneo yenye misitu kando ya miji mikubwa. Amesema,
Vurugu za kidini zaikumba shule Iringa, Tanzania
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Ifunda, iliyoko katika
Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini, jana walifanya vurugu kubwa
shuleni hapo na kutaka kumuua Mkuu wa shule hiyo, Bwana Shaaban Nsute.
Katika vurugu hizo ambazo zilianza juzi jioni na kuendelea hadi saa tano
usiku, wanafunzi hao ambao walivalia kininja na kuficha sura zao wakiwa
na visu mkononi, walivunja vioo vya madirisha shuleni hapo. Wanafunzi
hao wanadaiwa kumfuata mkuu wa shule hiyo Bwana Nsute nyumbani kwake
lakini alikimbia na kwenda kujificha kwenye shamba la mahindi ambapo
wanafunzi hao walimpiga mlinzi wa shule Bwana Yasini Luhala kwa mawe
akiwa katika ofisi yake. Nsute alisema vurugu hizo ambazo zimedhibitiwa
pia na Jeshi la Polisi zilizuka wakati mwanafunzi mmoja wa Kiislamu
aliyevaa kofia ya kidini kudhalilishwa na mlinzi wa shuleni hiyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)