Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, September 20, 2012

Al Azhar yalaani kuvunjiwa heshima Mtume SAW



Al Azhar yalaani kuvunjiwa heshima Mtume SAW Shekhe Mkuu wa Al Azhar, Ahmed al-Tayyeb amelaani vikali hatua ya jarida moja la Ufaransa kuchapisha tena vijikatuni vinavyomdhalilisha na kumtusi Nabii Muhammad SAW.
Vijikatuni hivyo vimechapishwa katika jarida la kila wiki la Charlie Hebdo la Ufaransa. Wakati huo huo Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imetoa wito kwa Waislamu kote duniani kufanya maandamano makubwa ya amani ya kulaani uchapishaji wa vijikatuni hivyo.
Jarida hilo la Ufaransa limethubutu kufanya kitendo hicho kichafu huku Waislamu wakiendelea kuandamana kote duniani kulaani utengenezaji wa filamu inayomvunjia heshima Mtume SAW huko Marekani.

No comments:

Post a Comment