Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, September 30, 2012

Tahadhari ya UNHCR kuhusu Myanmar


Tahadhari ya UNHCR kuhusu Myanmar
Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limetahadharisha juu ya hali mbaya inayowakabili Waislamu wa Myanmar. Taarifa ya UNHCR imeeleza kuwa, karibu Waislamu elfu sabini na tano wanaishi katika mazingira hatarishi kwenye kambi za muda nchini humo. Waislamu hao wameamua kuhama makaazi yao na kukimbilia kwenye maeneo ya amani, baada ya Mabuda wenye misimamo ya kufurutu mipaka wakiungwa mkono na vikosi vya serikali ya nchi hiyo kuwasaka na kuwaua kwa halaiki. Taarifa zinaeleza kuwa, Waislamu hao wanakabiliwa na hali mbaya sana ya kiafya na lishe duni kwenye kambi zao za muda zilizoko umbali wa kilomita 500 kutoka mji mkuu wa nchi hiyo. Hata hivyo vitisho vingali bado vinaendelea vya watu wanaobeba silaha dhidi ya Waislamu laki nane walioko katika eneo la kaskazini mwa Myanmar. Watu hao wanaobeba silaha waliwaua kwa halaiki Waislamu wapatao 90 kutoka katika vijiji mbalimbali yapata miezi minne iliyopita.

No comments:

Post a Comment