Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, September 21, 2012

Sudan mbili zakubaliana kubadilishana wafungwa

Sudan mbili zakubaliana kubadilishana wafungwaSudan na Sudan Kusini zimekubaliana juu ya hatua ya ubadilishanaji wafungwa wa nchi mbili. Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Sudan Ibrahim Mahmood Hamid alipokutana na kamishna wa Sudan Kusini katika masuala ya ujenzi mpya na miundo mbinu mjini Khartoum. Viongozi hao wawili wamekubaliana kubadilishana wafungwa na kuwarejesha nchini mwao sambamba na kuhukumiwa kwa mujibu wa hukumu za nchi hiyo. Katika kikao hicho pia walijadili kuondolewa vizuizi vilivyopo kwa ajili ya kuwarejesha raia wa Sudan Kusini kutoka nchini Sudan. Katika kipindi cha kujitenga Sudan Kusini kutoka Sudan kaskazini tarehe tisa mwezi Juni 2011, zilianza harakati za kuwahamisha raia wa nchi mbili katika maeneo yao ya asili, suala lililopelekea maelfu ya raia wa nchi mbili hizo kurejea makwao.

No comments:

Post a Comment