Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, September 15, 2012

UN yatahadharisha kuhusu umaskini barani Afrika



UN yatahadharisha kuhusu umaskini barani AfrikaUmoja wa Mataifa umetahadharisha kuhusu umasikini katika nchi za kusini mwa jangwa kubwa la Afrika. David Gressly Mratibu wa Masuala ya Haki za Binadamu wa nchi za kandokando mwa jangwa la Sahara wa umoja wa Mataifa ameripoti kuwa, maisha ya watu milioni 50 yako hatarini kutokana na uwezekano wa kupungua mazao ya kilimo mwakani.
Gressly ameongeza kuwa kunyesha mvua katika nchi za kandokando mwa jangwa la Sahara ni ishara ya kuwepo mazao mazuri mwaka ujao hata hivyo kupungua kwa mazao na pia kupanda kwa bei za vyakula kutayaweka hatarini maisha ya watu milioni kumi wa eneo hilo.
Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu katika nchi za kandokando mwa jangwa la Sahara wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, tayari wameandaa mpango wa kupunguza lishe duni kwa watoto wa Kiafrika  milioni moja. Hii ni katika hali ambayo, mwaka uliopita watoto laki tano wa Kiafrika walikuwa wakisumbuliwa na tatizo la lishe duni.

No comments:

Post a Comment