Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, September 29, 2012

Waislamu Ethiopia waandamana dhidi ya serikali

Waislamu Ethiopia waandamana dhidi ya serikali

Maelfu ya Waislamu wa Ethiopia wamefanya maandamano makubwa kwenye miji mbalimbali ya nchi hiyo wakipinga siasa za serikali ya Adiss Ababa. Waislamu wa Ethiopia wanaituhumu serikali ya nchi hiyo kwa kuingilia kati masuala ya dini hiyo na hali kadhalika ikifanya njama za kuwashinikiza Waislamu wafuate mikikati iliyopangwa na serikali. Malalamiko ya Waislamu dhidi ya siasa na sera za serikali ya nchi hiyo yameanza tokea miezi tisa iliyopita. Waandamanaji walilaani vikali mipango ilyoratibiwa na serikali ya kuwachagulia viongozi wa kidini kinyume na irada na matakwa ya Waislamu walio wengi nchini humo. Hali kadhalika waandamanaji wametaka waachiliwe huru vingozi wao wanaoshikiliwa na vyombo vya dola nchini humo.

No comments:

Post a Comment