Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, September 24, 2012

Al Shabab yakiri kumuua mbunge wa Somalia

Al Shabab yakiri kumuua mbunge wa Somalia Wanamgambo wa kundi la al Shabab wa Somalia wamesema kuwa wao ndio waliomfyatulia risasi na kumuua mbunge wa Somalia hapo jana na kutishia kumuua kila mbunge wa nchi hiyo. Watu waliokuwa na silaha jana walimuua kwa kumfyatulia risasi Mustafa Haji Mohamed nje ya nyumba yake baada ya sala ya Ijumaa. Sheikh Abdiasis Abu Musab msemaji wa oparesheni za kijeshi wa kundi la wanamgambo wa al Shabab amesema kwa kuhoji kuwa ni mara ngapi wamewaonya Wasomalia kujiunga na serikali ya kikafiri? Msemaji wa al Shabab amesema wamemuua mbunge Mustafa na kwamba watawaua wabunge wote na maafisa wa Somalia. Augustine Mahiga Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia ameyaelezea mauaji ya mbunge huyo yaliyofanywa na al Shabab kuwa ni kitendo cha woga kinachokumbusha changamoto zinazozikabili taasisi mpya na uongozi wa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment