Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, September 29, 2012

Ikhwan: Hakuna mwafaka kati ya Israel na Misri

Ikhwan: Hakuna mwafaka kati ya Israel na Misri

Katibu Mkuu wa Harakati ya Ikhwaanul Muslimiin nchini Misri amesema kuwa, Rais Muhammad Mursi wa nchi hiyo hatakutana na kufanya mazungumzo na kiongozi yeyote wa utawala wa Kizayuni wa Israel. Mahmoud Hussein amesema kuwa, Rais Mursi hatakutana na kiongozi yeyote wa utawala wa Israel hata kama ikiwa ni kuufanyia marekebisho mkataba wa amani wa Camp David. Mahmoud Hussein amesisitiza juu ya kukomeshwa uchokozi unaofanywa na utawala huo ghasibu dhidi ya wananchi wa Palestina wa eneo la Ukanda wa Gaza, sanjari na kusimamishwa kikamilifu ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Katibu Mkuu wa Ikhwaanul Muslimiin amesema, hakuna kiongozi yeyote wa Misri atakayefanya mazungumzo na kiongozi wa Israel hadi pale zitakapodhaminiwa haki za wananchi wa Palestina.

No comments:

Post a Comment