skip to main |
skip to sidebar
Kufunguliwa mpaka kati ya Kodivaa na Ghana
Mpaka wa anga kati ya Ivory Coast na Ghana ambao ulikuwa
umefungwa kufuatia mashambulizi ya watu wenye silaha dhidi ya wanajeshi
wa Ivory Coast sasa umefunguliwa. Ofisi ya Rais wa Ivory Coast
imetangaza kuwa mpaka wa anga kati ya nchi hiyo na Ghana umefunguliwa
kuanzia leo. Hata hivyo mpaka wa nchi kavu kati ya nchi mbili hizo ambao
ulifungwa kufuatia mashambulizi hayo umeendelea kufungwa.
Serikali ya
Ivory Coast imeyahusisha mashambulizi hayo ya karibuni dhidi ya
wanajeshi wa nchi hiyo na watu waliokuwa na silaha ambao walivuka mpaka
na kuingia Kodivaa kutokea Ghana. Ivory Coast ilifunga mipaka ya anga na
nchi kavu kati yake na Ghana tangu Ijumaa iliyopita. Waziri wa Mambo ya
Ndani wa Ivory Coast amesema kuwa mashambulizi hayo yamefanywa na
wafuasi wa Laurent Gbagbo Rais wa zamani wa nchi hiyo ambao walikimbilia
nchini Ghana.
No comments:
Post a Comment