Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, September 25, 2012

Kufunguliwa mpaka kati ya Kodivaa na Ghana



Kufunguliwa mpaka kati ya Kodivaa na Ghana Mpaka wa anga kati ya Ivory Coast na Ghana ambao ulikuwa umefungwa kufuatia mashambulizi ya watu wenye silaha dhidi ya wanajeshi wa Ivory Coast sasa umefunguliwa.  Ofisi ya Rais wa Ivory Coast imetangaza kuwa mpaka wa anga kati ya nchi hiyo na Ghana umefunguliwa kuanzia leo. Hata hivyo mpaka wa nchi kavu kati ya nchi mbili hizo ambao ulifungwa kufuatia mashambulizi hayo umeendelea kufungwa.
Serikali ya Ivory Coast imeyahusisha mashambulizi hayo ya karibuni dhidi ya wanajeshi wa nchi hiyo na watu waliokuwa na silaha ambao walivuka mpaka na kuingia Kodivaa kutokea Ghana. Ivory Coast ilifunga mipaka ya anga na nchi kavu kati yake na Ghana tangu Ijumaa iliyopita. Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ivory Coast amesema kuwa mashambulizi hayo yamefanywa na wafuasi wa Laurent Gbagbo Rais wa zamani wa nchi hiyo ambao walikimbilia nchini Ghana.

No comments:

Post a Comment