Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, September 15, 2012

Hizbullah: Yaitisha maandamano makubwa Lebanon

Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imeitisha maandamano makubwa zaidi nchini humo kulaani hatua ya kuvunjiwa matukufu ya dini ya Kiislamu.
Hizbullah: Yaitisha maandamano makubwa LebanonMaandamano hayo yenye lengo la kutetea matukufu ya Kiislamu yanatarajiwa kufanyika Jumatatu ijayo mjini Bairut, Lebanon. Hivi karibuni pia Waislamu mjini Bairut walifanya maandamano makubwa wakilaani filamu iliyomtusi mtukufu Mtume Muhammad (sww) na kuutaka ulimwengu wa Kiislamu uchukue hatua kali za kukabiliana na njama za Marekani. Aidha hapo jana raia mmoja wa Lebanon aliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya waandamanaji waliokuwa wamejawa na hasira kali kutaka kuvamia hoteli moja ya Kimarekani nchini humo. Mbali na Lebanon nchi nyingine za Kiislamu kamavile Misri, Libya, Bahrain, Tunisia, Yemen, Iran, Indonesia na Palestina zilishuhudia maandamano makubwa huku idadi ya watu wakiuawa na kujeruhiwa vibaya.

No comments:

Post a Comment