Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, September 13, 2012

Mafuriko na kipindupindu vyaua watu 160 Nigeria



Duru za habari kutoka Nigeria zinaarifu kuwa, mafuriko yaliyosababishwa na kunyesha mvua kubwa tangu mwezi Juni hadi mwezi huu nchini humo, yamepelekea kuuawa watu 160. Ripoti iliyotolewa na ofisi inayoshughulikia masuala ya kibinaadmu ya Umoja wa Mataifa yenye makao yake makuu mjini Niamey, Niger imetangaza kuwa, takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa zaidi ya watu laki tano na 27 elfu wameathiriwa na mafuriko hayo huku watu 81 wakipoteza maisha yao. Awali viongozi Nigeria walikuwa wametoa  ripoti iliyoonyesha kuuawa watu 68 na wengine laki nne na 85 elfu wakiathiriwa vibaya na mafuriko hayo. Aidha ripoti iliyotolewa na ofisi inayoshughulikia masuala ya kibinaadmu ya Umoja wa Mataifa imeashiria kuwa watu wengine 81 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa kipindupindu uliyoyakumba maeneo ya magharibi mwa nchi hiyo na kufanya idadi ya watu waliopoteza maisha yao kufikia 160.

No comments:

Post a Comment