Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, September 17, 2012

Watu 45 wauawa katika mapigano nchini Somalia


Watu wasiopungua 45 wameuawa na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa katika mapigano yaliyotokea kusini mwa kijiji cha Bibi kati ya majeshi ya Kenya na Somalia kwa upande mmoja dhidi ya wapiganaji wa kundi la al Shabaab.
Watu 45 wauawa katika mapigano nchini Somalia
Mapigano hayo yametajwa kuwa ndiyo makali zaidi kutokea huko kusini mwa Somalia tangu majeshi ya Kenya yaingie nchini humo mwezi Oktoba mwaka jana.
Mapigano baina ya pande hizo mbili yalishadidi zaidi baada ya jaribio la majeshi ya Kenya na Somalia la kutaka kuingia katika ngome za kundi la al Shabaab karibu na kijiji cha Bibi.
Hadi sasa hakujatolewa habari kamili kuhusu idadi kamili ya watu waliouwa katika mapigano hayo kutoka pande zote mbili lakini vyombo vya kuaminika vinasema makumi ya watu wameuawa.
Duru za kundi la al Shabaab zinasema kuwa ndege za kijeshi za Kenya zinashiriki katika mapigani hayo makali.

No comments:

Post a Comment