Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, September 30, 2012

Kamanda wa waasi Syria auawa na wafuasi wake

Kamanda wa waasi Syria auawa na wafuasi wake
Kamanda wa waasi wa Syria wanaoungwa mkono wa madola ya kigeni ameuawa na wafuasi wake wenye silaha waliomgeuka katika mji wa Dara'a. Rabea Swaidan aliuawa kwenye mji huo kusini mwa Damascus hapo jana na wafuasi wake wakati walipokuwa wakigombania kugawana vitu walivyopora na fedha walizopokea kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao haramu. Wakati hayo yakiripotiwa vikosi vya serikali ya Syria vimedhibiti maeneo zaidi katika mji wa Aleppo yaliyokuwa yakikaliwa na magenge yenye silaha yanayoungwa mkono na madola ya nje, huku waasi 180 wakiuawa na wengine 30 kukamatwa. Maeneo hayo yamedhibitiwa katika operesheni kubwa ya kijeshi ya serikali dhidi ya waasi wanaopigana dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad wa Syria.

No comments:

Post a Comment