Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, September 20, 2012

Sudan mbili kukamilisha mazungumzo Ethiopia



Sudan mbili kukamilisha mazungumzo EthiopiaRais Omar Hassan al-Bashir wa Sudan anatarajiwa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na mwenzake wa Sudan Kusini Salva Kiir siku ya Jumapili wakati wa kikao cha mwisho cha pande mbili ambacho kimechukua muda wa majuma mawili. Kikao hicho kilichowashirikisha wawakilishi kutoka Juba na Khartoum kililenga kutatua mivutano kati ya serikali mbili hizo kuanzia suala la ugawanaji sawa wa pato la mafuta hadi kadhia ya usalama wa mipakani. Mkuu wa timu ya Mazungumzo ya Sudan Kusini, Pagan Amum amethibitisha kuwa kikao hicho kitafanyika mjini Addis Ababa. Mjumbe maalum wa Norway huko Sudan na Sudan Kusini, Endre Stiansen amesema jamii ya kimataifa imefurahishwa na jinsi mazungumzo ya pande mbili yalivyokwenda ndani ya majuma mawili yaliyopita na kwamba Umoja wa Mataifa una matumaini ya kusainiwa makubaliano ya kudumu kati ya Sudan na Sudan Kusini kuhusu usalama wa mpakani wakati wa mkutano wa Jumapili kati ya Marais Omar al-Bashir na Salva Kiir. 

No comments:

Post a Comment