
Watu walioshuhudia wameeleza kuwa sauti ya milipuko mitatu mikubwa imesikika mapema leo katika jengo hilo la maduka la Westgate jijini Nairobi.
Vikosi vya Kenya vinajaribu kupambana na wanamgambo wa as Shabab waliovamia jengo hilo la biashara juzi Jumamosi ambalo sehemu yake moja imetajwa kumilikiwa na Israel. Katika mashambulizi hayo ya as Shabab, karibu watu 70 wameuawa na wengine wanaokaribia 200 kujeruhiwa sambamba na kushikwa mateka wengine wengi.
No comments:
Post a Comment