Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, September 24, 2013

Asasi za Kiislamu zaitaka Nigeria kuchunguza mauaji

Asasi za Kiislamu zaitaka Nigeria kuchunguza mauaji

Taasisi za Kiislamu na za kutetea haki za binadamu nchini Nigeria zimeitaka serikali ya Abuja kufanya uchunguzi kuhusiana na mauaji ya makumi ya watu wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram. Jumuiya hizo zimeashiria mauaji ya hivi karibuni ya makumi ya watu mjini Abuja wanaoshukiwa kuwa wanachama wa Boko Haram na kusisitiza kwamba, kuna utata katika tukio hilo hivyo kuna haja ya kufanyika uchunguzi wa kina kuhusiana na mauaji hayo. Taasisi za Kiislamu na za kutetea haki za binadamu nchini Nigeria zimetangaza kuwa, kuna udharura wa kufanyika uchunguzi kuhusiana na mauaji hayo. Wakati huo huo, Taasisi ya Kitaifa ya Haki za Binadamu nchini Nigeria imetangaza kuwa, uchunguzi kuhusiana na mauaji hayo tayari umeshaanza. Kundi la Boko Haram linahusishwa na mashambulio mengi ya kigaidi nchini Nigeria. Boko Haram ni kundi lenye misimamo ya kufurutu mipaka nchini Nigeria ambalo kutokana na kuwa na ufahamu mbaya na potofu kuhusiana na Uislamu, limeitumbukiza nchi hiyo katika dimbwi la machafuko na mauaji sambamba na kuzusha hitilafu za kidini na kikabila nchini humo

No comments:

Post a Comment