Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, September 18, 2013

Mali za wakuu wa Ikhwanul Muslim zazuiwa Misri


Mali za wakuu wa Ikhwanul Muslim zazuiwa MisriMahakama ya jinai ya Misri imekubaliana na suala la kuzuiwa mali za baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa harakati ya Ikhwanul Muslimin ya nchini humo kwa tuhuma za mauaji na kuchochea machafuko.
Mahakama ya jinai ya Misri Jumanne hii imeafiki ombi lililokuwa limewasilishwa na mwendesha mashtaka mkuu wa nchi hiyo kwa ajili ya kuzuiwa mali za viongozi na maafisa wa ngazi ya juu wa Ikhwanul Muslimin.
Hisham Barakat mwendesha mashtaka wa Misri, awali aliiomba mahakama ya jinai ya nchi hiyo ikubali kuzuiwa mali za viongozi kadhaa wa ngazi za juu wa harakati ya Ikhwanul Muslimin kutokana na tuhuma hizo wakiwemo Muhammad Badie kiongozi wa kundi hilo,  naibu wake Khairat Shater, Mahmud Izzat Ibrahim, Mahdi Akef, Mohamed Saad al Katatni, Rashad al Bayumi, Issam al Aryan na viongozi wengine kadhaa wa ngazi ya juu wa harakati hiyo. 
Viongozi wengi wa Ikhwanul Muslimin wametiwa mbaroni katika maeneo mbalimbali ya Misri baada ya wanajeshi wa nchi hiyo kumpindua madarakani Muhammad Morsi, Rais halali wa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment