Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, September 29, 2013

Mamlaka ya Ndani Palestina haitaki Intifadha


Mamlaka ya Ndani Palestina haitaki Intifadha
Idara za usalama za Mamlaka ya Ndani ya Palestina zimetangaza kuwa zinafanya kila linalowezekana ili kuzuia kuanza Intifadha ya Tatu huko katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Idara za usalama za Mamlaka ya Ndani ya Palestina zimedai kuwa kuanza Intifadha ya Tatu ya Wapalestina kutazusha hali ya hofu na wasiwasi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kwamba idara hizo zitafanya kila ziwezalo ili kuzuia kutokea intifadha hiyo. Mji wa Quds unaokaliwa kwa mabavu na Wazayuni pamoja na msikiti mtukufu wa al Aqswa ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu, Ijumaa iliyopita  ilishuhudia wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wakijenga vituo mbalimbali vya upekuzi sambamba na kujiri mapigano makali kati ya raia wa Kipalestina na wanajeshi wa Israel. Matukio hayo yalijiri baada ya harakati ya muqawama ya Palestina Hamas kutoa mwito kwa makundi mbalimbali ya wananchi wa Palestina huko katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na katika mji wa Quds wa kuunga mkono Intifadha ya Tatu ili kukabiliana na utawala wa Kizayuni. 

No comments:

Post a Comment