Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, September 5, 2013

Wito watolewa kusitisha mashambulio dhidi ya M23


Wito watolewa kusitisha mashambulio dhidi ya M23
Mawaziri wa Mambo ya Nje waEneo la Maziwa Makuu Barani Afrika wametaka kusitishwa mashambulio dhidi ya waasi wa M23 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ili kutoa mwanya kwa mazungumzo ya amani ya Kampala, Uganda.
Aidha wametaka kikosi cha uingiliaji cha Umoja wa Mataifa kuwashambulia waasi kutoka Uganda, Rwanda na Burundi ambao wanaendesha shughuli zao huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kati ya waasi hao ni wale wa FDLR, FNL na ADF.
Hayo yamebainika katika kikao cha faragha cha wakuu wa ulinzi na mawaziri wa mambo ya nje wa Eneo la Maziwa Makuu Barani Afrika waliokutana Kampala Jumatano usiku. Akizungumza baada ya kikao hicho Katibu wa Kudumu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Uganda Balozi James Mugune amesema machafuko katika eneo yanapaswa kutatuliwa kwa njia za amani. Leo Alkhamisi Viongozi wa Eneo la Maziwa Makuu Barani Afrika wanatazamiwa kukutana nchini Uganda kujadili hali ya Mashariki mwa Kongo. Nchi wanachama wa Kongamano la Kimataifa la Maziwa Makuu ni pamoja na Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Uganda, Rwanda, Sudan, Tanzania na Zambia.

No comments:

Post a Comment