Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, September 13, 2013

'Ndege isiyo na rubani kutopelekwa sasa Kongo'


'Ndege isiyo na rubani kutopelekwa sasa Kongo'Umoja wa Mataifa umesema kuwa mpango wake wa kupeleka ndege ya kijasusi isiyo na rubani huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umecheleweshwa kwa miezi kadhaa.Ndege hiyo itapelekwa katika eneo la Kongo lililoko karibu na mpaka wa Rwanda.
Vilevile Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetangaza kuwa, licha ya kurejea nyuma waasi wa M23 huko Mashariki mwa Kongo lakini bado eneo hilo halina amani na usalama. Marry Robinson, Mwakilishi maalum wa UN katika eneo la Maziwa Makuu ameliomba baraza hilo lizishinikize nchi za Rwanda, Kongo, Uganda na Burundi zifanye mazungumzo ili kuimarisha amani na usalama wa kudumu kwenye eneo hilo.

No comments:

Post a Comment