Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, September 14, 2013

Mripuko wa guruneti watikisa jiji la Kigali, Rwanda

Mtu mmoja ameuawa na wengine 14 kujeruhiwa baada ya kutokea mripuko wa guruneti, Kigali mji mkuu wa Rwanda. Mripuko huo umetokea zikiwa zimesalia siku tatu kabla ya kufanyika uchaguzi wa bunge nchini humo. ACP Damas Gatare Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Rwanda amesema kuwa, watu watatu wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuhusika na mripuko huo. Hadi sasa hakuna mtu au kikundi chochote kilichojitangaza kuhusika na mripuko huo. Viongozi wa Rwanda wametangaza kuwa, miezi ya Julai na Agosti ilijiri miripuko miwili ya maguruneti mjini Kigali, na kulituhumu kundi la  waasi wa FDRL walioko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kutekeleza shambulio hilo. Uchaguzi wa Rwanda umepangwa kufanyika siku ya Jumatatu, huku chama tawala cha Rwanda Patriotic Front (RPF) kinachoongozwa na Rais Paul Kagame kinatarajiwa kuibuka na ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi huo.

No comments:

Post a Comment