Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, September 19, 2013

BAADA YA KUSUBIRI KWA MIAKA 44, HATIMAYE MSIKITI WA KWANZA KUJENGWA SLOVENIA

jiwe la msingi wa msikiti  kwanza nchini Slovenia kujengwa limewekwa katika mji mkuu wa zamani wa viwanda wa Ljubljana siku ya Jumamosi. Hatua hii imekuja zaidi ya miaka 44, tangu waislamu walipopeleka maombi ya kwanza rasmi ya kutaka kuwa na eneo rasmi kwa ajili ya ibada.

Mpango wa ujenzi wa msikiti umekuwa unakabiliwa na vikwazo vya utawala na ukosefu wa utashi wa kisiasa katika nchi hiyo yenye wakatoliki milioni mbili, ambapo idadi ya waislamu ni 50,000 tu.

Takribani watu 10,000 walihudhuria sherehe za uwekaji jiwe la msingi la msikiti, akiwemo waziri mkuu wa Slovenia bi Alenka Bratusek, waziri wa serikali ya Qatar ambayo inafadhili mradi huo na Meya wa Ljubljana, Zoran Jankovic, ambao kwa pamoja walisaidia kuweka jiwe la msingi. Wanawake wachache waliovaa hijabu walihudhuria  katika uzinduzi wa msikiti huo.

Waziri mkuu huyo wa Slovenia aliuambia umati uliohudhuria kwamba ni ishara ya ushindi wa kila aina ya uvumilivu uliooneshwa na waislamu katika kipindi chote cha kukosa msikiti na kuongeza kwamba ulaya bila kuwa na uislamu haiwezi kuwa tajiri.

"Hii ina maana dunia ni yangu ," alisema Sahra Kacar , 44, ambaye alizaliwa mwaka ambao yalipelekwa maombi ya kwanza rasmi ya kujenga msikiti katika Ljubljana. "Tutakuwa na mahali sahihi pakufanyia ibada, badala ya kutumia kumbi mbalimbali za umma ." Alisema


Ombi la ujenzi wa msikiti lilikuwa  linashikiliwa na maafisa wa mitaa, ambao baadhi yao walijaribu kulazimisha kura ya maoni juu ya suala hilo mwaka 2004. Watu 12,000 walisaini ombi la wito wa kura ya maoni ili pasi jengwe msikiti, lakini Mahakama ya Katiba ya Slovenia ilikataa kwa kusema itakuwa ni kinyume na katiba kwa misingi ya uhuru wa dini.

" Tunafuraha kwa kuanza ujenzi huu Ljubljana , ambao utakuwa bora na utakaojulikana na mji zaidi," Mufti Nedzad Grabus , Kiongozi wa juu wa jamii ya Kiislamu ya Slovenia , aliiambia sherehe.
Ujenzi wa msikiti unatarajiwa kuanza kwa kasi Novemba mwaka huu na unatarajiwa kuchukua miaka mitatu kwa gharama ya dollar milioni 12. Asilimia 70 ya fedha zitatolewa na serikali ya Qatar.

Mradi huo umekuja wakati Slovenia ipo katika hali mbaya ya kifedha tangu uhuru wa mwaka 1991, ambapo unatishia taifa kutafuta fedha kutoka EU na Shirika la Fedha Duniani .Mradi wa ujenzi wa msikiti huo umewafanya baadhi ya wasio kuwa waislamu kukasirika na kulaumu maamuzi ya kukubali kujengwa.

"Mimi binafsi sina chuki dhidi ya msikiti lakini najua watu ambao bado wana chuki dhidi yake ," alisema designer mwenye umri wa miaka 30 ambaye anaishi karibu na msikiti mpya,alitoa jina lake moja la Ana.


No comments:

Post a Comment