Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, September 7, 2013

WAANDAMANA KUPINGA MISS WORLD,INDONESIA

Maelfu ya waandamanaji wamejitokeza mwanzoni mwa wiki hii kupinga  mashindano ya Miss World yanayotarajia kuanza jumapili ya kesho nchini Indonesia .Waandamanaji hao wametaka shindano hilo lifutwe kwani linadhalilisha utu wa mwanamke na ni kinyume na mafundisho ya kiislamu.
Upinzani mkubwa toka kwa waandamanaji hao umezidi, katika taifa hilo lenye  Waislamu wengi zaidi duniani,licha ya waandaaji kudai wameondosha vazi la ufukweni (bikini)

Baadhi ya wanaume na wanawake 800 kutoka kundi la Hizbut Tahrir la Indonesia wamekusanyika katika mji wa Jakarta nje ya wizara ya ustawi wa jamii, wakitoa wito kwa serikali wa kufuta shindano hilo.
Aidha waliandamana hadi makao makuu ya shirika la habari la Indonesia MNC kwamba liache kutangaza habari za shindano hilo lililopotoka. "Je, tunataka nchi yetu kuonekana kama ya watu wa ngono?" mmoja wa waandamaji alisema kwa sauti kubwa .

"Sisi tutaendelea kuandamana na kuwaambia watu jinsi ya udhalilishaji wanawake kwa kufanyika shindano hili," alisema mratibu wa maandamano hayo,  Zikra ASRI,huku akiwa amezungukwa na wanawake  waliovaa hijabu nyeupe na baibui nyeusi.

Mjini Medani katika kisiwa cha Sumatra,  wanachama 500 wa Hizbut Tahrir waliandamana hadi majengo ya serikali, na kudai kuwa shindano hilo lifutwe.Licha ya upinzani kuongezeka , waandaaji wamesema kuwa  shindano hilo lazima lifanyike na halita athiri heshima na utamaduni wa indonesia
Shindano la Miss Dunia linatarajiwa kuanza Jumapili katika kisiwa cha Bali, na mshindi anatarajiwa kupatikana  katika jiji la Jakarta Septemba 28.

Nchi hiyo yenye watu milioni 240,June mwaka jana mwanamuziki Lady Gaga alilazimika kufuta onesho lake,baada ya viongozi wa dini ya kiislamu kutishia kuchoma moto ukumbi ambao atafanyia onesho hilo,baada ya mwanamuziki huyo kuonesha mavazi yake ya ndani.
waandamanaji nchini indonesia

No comments:

Post a Comment