Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, September 18, 2013

Suala la samaha kwa M23 kujadiliwa Kampala


Suala la samaha kwa M23 kujadiliwa KampalaMazungumzo mapya ya amani kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kngo na waasi wa M23 mjini Kampala Uganda yanatarajiwa kujadili mambo mengi lakini kubwa zaidi ni msamaha kwa waasi hao. Waziri wa Ulinzi wa Uganda, Crispus Kyonga ambaye alifungua upya mazungumzo hayo hapo jana amesema makubaliano ya mwisho yatafikiwa karibuni hivi. Ajenda za mazungumzo hayo ni namna ya kuwarudisha waasi wa M23 jeshini sanjari na kuhakikisha kwamba wakimbizi waliotoroka kufuatia machafuko wanarudi katika maeneo yao. Dkt. Kyonga ambaye ndiye mpatanishi wa mgogoro huo amesema serikali ya Kinshasa na waasi wana azma ya kufikia mapatano na kusitisha machafuko na uasi mashariki mwa nchi. Mazungumzo ya Kampala yalivunjika miezi kadhaa iliyopita baada ya Umoja wa Mataifa kuidhinisha kikosi maalumu cha kikanda kuenda mashariki mwa DRC kwa lengo la kupambana na makundi ya waasi hususan waasi wa M23 ambao mwaka uliopita waliuvamia na kuuteka mji wa kistratejia wa Goma.

No comments:

Post a Comment