Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, September 29, 2013

Viongozi wa Iraq walaani mashambulizi ya Arbil


Viongozi wa Iraq walaani mashambulizi ya Arbil
Ofisi ya Waziri Mkuu wa Iraq imelaani miripuko ya mabomu iliyotokea leo katika mji wa Arbil wa kaskazini mwa nchi hiyo.
Ali al Musawi, Mshauri wa Masuala ya Habari wa Waziri Mkuu wa Iraq, Noor al Maliki, amesema leo jioni kuwa, serikali ya nchi hiyo inalaani vikali miripuko iliyotokea kwenye mji wa Arbil huko Kurdistan Iraq na kupelekea watu 6 kuuawa na wengine 38 kujeruhiwa.
Al Musawi aidha ameashiria namna mgogoro wa Syria unavyohatarisha pia usalama wa nchi jirani hasa Iraq na kusema kuwa, miripuko hiyo ya mabomu ina uhusiano na matukio ya Syria.
Leo Jumapili kumetokea miripuko mitano ya mabomu mbele ya ofisi ya usalama ya mjini Arbil, kaskazini mwa Iraq, sambamba na kutangazwa ushindi wa chama cha Democrat cha Kurdistan ya Iraq kinachoongozwa na Masoud Barzani.

No comments:

Post a Comment