Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, September 24, 2013

Kenya: Tunaidhibiti Westgate, operesheni iko ukingoni


Kenya: Tunaidhibiti Westgate, operesheni iko ukingoniSerikali ya Kenya imetangaza kuwa, vikosi vya usalama vya nchi hiyo vinadhibiti jengo la madula la Wesgate lililokuwa likidhibitiwa na magaidi wa kundi la wanamgambo wa al-Shabab. Taarifa ya serikali ya Kenya imesema kuwa, kwa sasa vikosi vya usalama vinapambana na gaidi mmoja au wawili ambao wamebakia katika jengo hilo. Manoah Esipisu, Msemaji wa serikali ya Kenya ametangaza kwamba, vikosi maalumu vya usalama vilivyoko katika eneo hilo vinaendelea kusonga mbele bila upinzani mkubwa. Aidha amesema kuwa, mateka wote waliokuwa wakishikiwa na magaidi hao wamekombolewa na kwa sasa inafanyika operesheni ya kumaliza kabisa tukio hilo lililodumu kwa siku tatu. Hadi sasa inaelezwa kuwa, watu wasiopungua 69 wameuawa na wengine wasiopungua 200 kujeruhiwa.

No comments:

Post a Comment