Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Friday, September 13, 2013

Jeshi la Mali lapambana na waasi wa Tuareg


Jeshi la Mali lapambana na waasi wa Tuareg
Habari kutoka Mali zinasema kuwa, mapambano makali yameshuhudiwa kati ya wanajeshi wa serikali na waasi wa Tuareg katika mji wa Lere katikati mwa nchi hiyo. Duru za habari zinaripoti kuwa, waasi hao ndio walioanza kuwashambulia wanajeshi wa serikali kuanzia jana Jumatano ingawa wao wamedai jeshi ndilo lililoanza kuwafyatulia risasi na makombora ya mizinga. Makabiliano hayo yamepelekea waasi kadhaa kuuawa huku wanajeshi 3 wa serikali wakijeruhiwa vibaya. Hii ni mara ya kwanza kwa vita kama hivyo kutokea tangu pande mbili hizo kusaini makubaliano ya amani mwezi Juni mwaka huu. Vita hivyo aidha vinatokea ikiwa imepita wiki moja tu tangu rais mpya, Ibrahim Keita ashike rasmi hatamu za uongozi wa nchi hiyo ya mgharibi mwa Afrika; jambo linaloashiria kibarua kigumu kinachomsubiri kiongozi huyo katika juhudi zake za kutafuta maridhiano ya kitaifa.

No comments:

Post a Comment