Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, September 18, 2013

Sudan yatishia kukata kabisa uhusiano na Marekani


Sudan yatishia kukata kabisa uhusiano na Marekani
Serikali ya Sudan imetishia kukata kabisa uhusiano wa kidiplomasia na Marekani iwapo Washington itaendeleza siasa zake za kijuba dhidi ya Khartoum. Indhari ya Sudan inafuatia hatua ya Marekani ya kumzuia Rais Omar Hassan al-Bashir kuhudhuria mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa utakaoanza Jumapili ijayo mjini New York. Rais Bashir alikuwa ameomba rasmi viza ya kusafiri Marekani kuhudhuria mkutano huo lakini Washington ikalaani hatua hiyo na kusema Bashir anapaswa kusafiri Uholanzi na kujisalimisha mbele ya mahakama ya ICC na wala sio kwenda Umoja wa Mataifa. Sasa serikali ya Sudan kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imesema itamfukuza balozi wa Marekani mjini Khartoum na pia kusimamisha biashara ya mafuta na Sudan Kusini iwapo Washington haitobadili misimamo yake. Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imesema Marekani haipaswi kuzungumzia suala la haki za binadamu kwani rekodi yake katika uwanja huo ni mbovu na yenye kutoa uvundo.

No comments:

Post a Comment