Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Thursday, September 5, 2013

UN: Mgogoro wa Syria ni mkubwa mno


UN: Mgogoro wa Syria ni mkubwa mnoUmoja wa Mataifa umesema kuwa watu elfu sita wanaikimbia Syria kila siku kutokana na kushadidi mapigano nchini humo. Hayo yalisemwa jana katika kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani. Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa Masuala ya Wakimbizi wa Umoja wa Mataifa amesema katika kikao hicho kuwa kamisheni yake haijawahi kuona idadi ya wakimbizi ikiongezeka kwa kiwango cha kutisha namna yote hiyo tangu miaka 20 iliyopita. Ivan Simonovic, Naibu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya haki za binadamu amedai kuwa, watu wasiopungua 92,901 waliuawa huko Syria kati ya mwezi Machi mwaka juzi hadi mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka huu, miongoni mwao wakiwemo watoto zaidi ya 6,500. Amesema, inakadiriwa kuwa watu elfu tano wanauawa huko Syria kila mwezi. Serikali ya Damascus inasema kuwa, madola ya kigeni ambayo hayaitakii kheri Syria yamepeleka makundi ya kigaidi na kuyasaidia kwa kila hali ili yafanye mauaji ya raia na maafisa wa serikali nchini humo.

No comments:

Post a Comment